Posts

Showing posts from August, 2014

TETESI ZA SOKA ULAYA

Image
Real Madrid wamekamilisha uhamisho wa pauni milioni 20 wa Radamel Falcao, 28, kutoka Monaco (Calciomercato), Arsenal wana matumaini ya kukamilisha uhamisho wa beki Sorkatis Papastathopoulos, 26, kutoka Borussia Dortmund, lakini wamesema hawatalipa pauni milioni 20 (Daily Mirror), boss wa Aston Villa Paul Lambert ametoa dau la pauni milioni 8 kumtaka kiungo wa Manchester United Tom Cleverly, 25, (Daily Telegraph), lakini Lambert huenda wakapata upinzani mk ali kutoka Valencia, ambao nao pia wamepanda dau kwa Cleverly (Sky Sports),  Danny Welbeck, 23, anajiandaa kuondoka Old Trafford, na akitajwa kwenda Tottenham kwa mkopo (Daily Star), Chelsea wanakaribia kutoa ruhusa kwa Fernando Torres, 30, kwenda A.C Milan (Times) , Manchester United wameongeza bidii kumfuatilia kiungo Martin Odegaard, 15, anayechezea Stromsgodset kutoka Norway (Daily Telegraph), Valencia na Juventus wametoa dau la kutaka kumsajili Javier Hernandez, 26, kutoka Manchester United kwa kiasi cha pauni milioni 15 (Gu...

TETESI ZA SOKA ULAYA

Image
Boss wa Manchester United Louis van Gaal anajaribu kumnunua kiungo wa Juventus Arturo Vidal, 27, na beki wa Ajax Daley Blind, 24, kabla ya dirisha la usajili kufungwa Septemba mosi (Daily Mirror), United watalazimika kulipa pauni milioni 20 kumsajili Blind (Sun), Liverpool bado wanajaribu kumfuatilia kiungo wa zamani wa Arsenal Alex Song, 26, ambaye yuko Barcelona (Metro), meneja wa Arsenal, Arsene Wenger amesema hatotaka kuwasajili Danny Welbeck, 23, kutoka Man U, Radamel Falcao kutoka Monaco, 28, na Nikola Zigic, 33, kutoka Birmingham  (London24.com), Manchester United watapanda dau la pauni milioni 24 kwa kiungo wa Sporting Lisbon William Carvalho, 22, wakati Louis van Gaal akitaka kuwaondoa Welbeck, Tom Cleverly, 25, na Shinji Kagawa, 25 (Daily Telegraph), Cleverly yuko tayari kusalia hadi mwaka ujao mkataba wake utakapokwisha (Independent), Sunderland wametoa dau la pauni milioni 6 kumsajili beki Virgil van Dijk, 23, kutoka Celtic baada ya Toby Alderweireld, 25 ...

DI MARIA RASMI MAN UTD

Image
                           ANGEL MIGUEL DI MARIA akipozi na Kocha mkuu wa Man utd LOUIS VAN GAL katika uwanja wa Old Trafford    

VIPODOZI FEKI HATARI TANI 7 VYATEKETEZWA MKOANI TANGA

Image
Tani 7 za vipodozi vinavyodaiwa kuwa na viambata vyenye sumu vimeteketezwa kwa moto katika dampo la mwang'ombe lililopo jijini Tanga kufuatia wakaguzi wa idara ya afya kufanya msako mkali na wa kushtukiza.  Katika baadhi ya maduka kisha kubaini kuuzwa kwa bidhaa hizo ambazo inadaiwa kuwa zimekuwa zikisababisha maradhi kwa watumiaji ikiwa ni pamoja na saratani ya ngozi. Mratibu anayesimamia masuala ya chakula na dawa wa halmashauri ya jiji la Tanga Bi. Alis Maungu amesema shehena hiyo ya vipodozi wameiteketeza ili kusaidia kupunguza madhara kwa watumiaji kwa sababu serikali imepiga marufuku bidhaa hizo kuuzwa madukani lakini baadhi ya wafanyabiashara bado wamekuwa wakikaidi agizo hilo. Amewatadharisha watumiaji hasa wanawake ambao wanaopenda kubadilisha ngozi zao kuwa nyeupe kuchukua tahadhari kwa sababu madhara ya vipodozi hivyo ni makubwa na yanajitokeza baadae kulingana na matumizi yake

FLORA MBASHA AFUNGUKA NA KUSEMA ANA MIMBA YA MBASHA NA SIO YA GWAJIMA

Image
Muimbaji wa nyimbo za Injili Tanzania ambae pia ni Mke wa Emmanuel Mbasha amefunguka na kusema kuwa hana mahusiano yoyote ya kimapenzi na na Mchungaji wa Kanisa la kanisa la Ufufuo na Uzima Josephat Gwajima, Muimbaji wa nyimbo za Injili Tanzania Flora Mbasha akichat Live katika ukurasa wa Facebook wa EATV leo jumatano. Flora amesema hayo leo alipokuwa akichat Live kupitia ukurasa wa Facebook wa EATV katika kipengele cha Kikaangoni Live kinachofanyika kila siku ya Jumatano kuanzia saa Sita kamili. Flora amesema kuwa hawezi kuwa na mahusiano ya kimapenzi na mtu ambae ni ndugu yake hivyo Mchungaji Gwajima ni mjomba wake na si mpenzi wake kama ambavyo watu wamekuwa wakizusha kwa lengo la kumchafua na kumshushia hadhi."Hayo ni maneno tu ya watu mtaani ila Mchungaji Gwajima ni mtumishi wa Mungu na ni uncle wangu ninawezaje kuwa na mahusiano na uncle wangu..? "Alihoji Flora. wakati akijibu ya maswali ya mashabiki ambayo mengi yao yalikuwa yakimtuhumu na h...

MAAJABU: TAZAMA MTI WA MAAJABU UNAOTOA MATUNDA YENYE UMBO KAMA LA BINADAMU

Image
Duniani kuna maajabu, mti huu unaotoa matunda yenye umbo la binadamu huko nchini Thailand na kuzaa kila baada ya miaka 20. Haya ndiyo maajabu ya dunia, ukistaajabu ya Musa utaona ya mti huu wa maajabu.

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI AKUTANA NA BALOZI WA CHINA NCHINI TANZANIA

Image
Naibu Waziri wa Nishati na Madini Mhe. Stephen Masele (kulia ) akizungumza na balozi wa China nchini Tanzania Dr. LU Youqing (kushoto) aliyemtembelea ofisini kwake leo kwa ajili ya maandalizi ya kongamano la China – Afrika linalotarajiwa kufanyika mkoani Arusha, Tanzania mapema Machi, 2015. Balozi wa China nchini Tanzania Dr. LU Youqing (kushoto) akizungumza na Naibu Waziri wa Nishati na Madini Mhe. Stephen Masele (kulia) juu ya hatua iliyofikiwa ya maandalizi ya kongamano hilo.